Serikali kukabiliana na wamiliki wa silaha haramu Trans nzoia magharibi
Serikali imewapa wakaazi wa Trans Nzoia magharibi hadi disemba kumi na tano kuwasilisha kwa mamlaka silaha wanazomiliki kinyume cha sheria.Mkuu wa wilaya hiyo Wilfred Kinyua ameonya kuwa yeyote atakae kosa kuitikia wito huo atachukuliwa hatua kali ya kisheria.Kinyua amedokeza kuwa eneo hilo limekumbwa na ukosefu wa usalama kutokana na watu wanaomiliki silaha hizo ambazo walizinunua kutoka nchi jirani.
Mkuu huo wa wilaya ambaye alikuwa akiandamana na mbunge wa Saboti Eugene Wamalwa amewataka wakaazi wa eneo hilo kushirikiana na maafisa wa usalama kwa kuripoti wahaalifu ambao wanaishi pamoja nao.