Nahodha wa klabu ya Arsenal Cesc Fabregas amekiri kufanya mazungumzo na aliyekuwa rais wa klabu ya Real madrid Ramon Calderon kwa simu.Calderon ambaye anapendezwa sana na kiwango cha usakataji soka wa Fabregas, kwa upande wake alisema alikuwa anamjulia hali mwanandinga huyo mzawa wa Uhispania jambo ambalo limewatia tumbo joto maafisa wakuu wa klabu hiyo.Fabregas mwenye umri wa miaka 21 anaenziwa sana na mibabe hao wa Uhispania lakini yuko na mkataba wa miaka mitano mingine na the gunners.Mazungumzo hayo ya Calderon na Fabregas yanajiri wakati msimu wa uhamisho wa wachezaji ukibisha hodi.
Mwisho Jimmy Kitiro
This entry was posted
on Wednesday, April 1st, 2009 at 10:44 am and is filed under Fahamu Ya Fish.
You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0 feed.
You can skip to the end and leave a response. Pinging is currently not allowed.