Archive for the 'Fahamu Ya Fish' Category

Wakulima wataka mahindi kununuliwa kwa shilingi 2360

Saturday, December 6th, 2008

Wakulima kutoka eneo la North Rift wametishia kutouzia mahindi yao shirika la kitaifa la mazao na nafaka nchini hadi pale nafaka yao yatanunuliwa kwa bei watakayokubaliana nayo.Mkulima maarufu ambaye pia ni mkurugenzi wa shirika la ukuzaji nafaka Timothy Busienei akizungumza kwa niaba ya wakulima alisema kuwa wakulima wanataka shirika la kitaifa la mazao na nafaka [...]

Masai ahimiza kanisa liwajibike kuhusiana na ukimwi

Monday, December 1st, 2008

Waumini na viongozi wa makanisa wana jukumu kusaidia taifa kukumbana na janga la Ukimiwi katika Wilaya ya Trans-Nzoia. Hayo yamesemwa na kiongozi wa Chama Cha Uzalendo katika eneo bunge la Cherangany, Bwana Jesse Masai, katika mashauri kuhusiana na janga hilo leo hii jijini Nairobi.Bwana Masai alisema Wakristo, katika sehemu hiyo yenye waumini wengi,wana jukumu la [...]

Fish united kukabiliana na Kimumu FC wikendi

Friday, November 28th, 2008

Klabu ya Fish United itachuana wikendi hii na Kimumu FC kwenye mechi za robo fainali katika kinyang’anyiro cha amani kinachoandaliwa na shiroka la ASTEP.Akizungumza na meza yetu ya michezo, kocha Lukas Lusigi alisema kuwa klabu hiyo ya Fish United ina imani kuwa itaibuka na ushindi katika mechi hiyo.
Lusigi amesema kuwa klabu hiyo imetia makali na [...]

Baraza la mji wa Eldoret kushirikiana na Morocco

Friday, November 28th, 2008

Baraza la manispaa ya mji wa Eldoret una mpango wa kuwa na ushirikiano wa muda mrefu na baraza la mji wa Rabat nchini Morocco. Meya wa mji wa Eldoret Sammy Rutoh amesema kuwa meya wa baraza hilo la Rabat Baron Omar ameahidi kufanya kazi kwa ushirikiano na manispaa ya mji wa Eldoret kwa kuiuza mji [...]

Kibaki aelekea Qatar kwa ziara rasmi ya siku tatu

Friday, November 28th, 2008

Rais Mwai Kibaki hii leo ataanza rasmi ziara ya siku tatu nchini Qatar. Rais pamoja na wajumbe watakaoandamana naye wanatarajiwa kuhudhuria kongamano la kimataifa kuhusu ufadhili na maendeleo. Rais Kibaki atakuwa miongoni mwa viongozi watakaokuwa wakijadili hali ya kusambaratika kwa uchumi dunianai. Inakisiwa kuwa hali hiyo ya kudorora kwa uchumi kwa sasa imeathiri mataifa mengi [...]

Serikali kukabiliana na wamiliki wa silaha haramu Trans nzoia magharibi

Tuesday, November 25th, 2008

Serikali imewapa wakaazi wa Trans Nzoia magharibi hadi disemba kumi na tano kuwasilisha kwa mamlaka silaha wanazomiliki kinyume cha sheria.Mkuu wa wilaya hiyo Wilfred Kinyua ameonya kuwa yeyote atakae kosa kuitikia wito huo atachukuliwa hatua kali ya kisheria.Kinyua amedokeza kuwa eneo hilo limekumbwa na ukosefu wa usalama kutokana na watu wanaomiliki silaha hizo ambazo walizinunua [...]

Kongamano kuangazia ripoti ya waki kufanyika Eldoret Alhamisi

Tuesday, November 25th, 2008

Mji wa Eldoret utaandaa kongamano siku ya Alhamisi wiki hii kwa madhumuni ya kujadili njia za kutekeleza mapendekezo ya ripoti ya Waki.Washika dau kutoka mkoa wa Bonde la ufa wanahofia kuwa juhudi za upatanishi na amani inayoendelezwa huenda ikakwama ikiwa swala kuhusu utekelezaji wa mapendekezo ya ripoti hiyo ya waki haitashughulikiwa ipasavyo.
Shirika la maendeleo [...]

Katiba mbaya yahitilafia shughuli za KACC

Tuesday, November 25th, 2008

Shirika la kupambana na ufisadi nchini KACC limesema kuwa ilikuwa vigumu kwao kuwachunguza na kuwashtaki wanasiasa wakuu humu nchini kutokana na hali ya sasa ya katiba.Mwenyekiti wa shirika hilo jaji Aaron Ringera amesema kuwa kesi zilizowasilishwa mbele ya tume yake haziwezi kuchunguzwa vikamilifu maana zilifutiliwa mbali na baadhi ya wahusika kutokana na sheria mbaya.Kwa sasa [...]

Watu 8 wavamiwa na uma mjini Eldoret.

Tuesday, November 25th, 2008

Washukiwa wanane wa wizi hii leo walivamiwa na kujeruhiwa na wananchi waliojawa na hasira katika jumba la Nandi Arcade mjini Eldoret.OCPD wa mji wa Eldoret Muinde Kioko amesema kuwa wanane hao ni baadhi ya  genge la wahalifu kumi na moja ambao wamekuwa wakiwahangaisha wakaazi wa mji wa Eldoret.Washukiwa hao walikuwa wamewaibia wakaazi wa mtaa wa [...]

Walimu watishia kufika katika afisi za elimu wilayani kuhusu kutolipwa kwa marupurupu yao

Tuesday, November 25th, 2008

Walimu wamekasirishwa sana na hatua ya tume ya kuwaajiri walimu nchini (TSC) ya kukosa kuwalipa pesa wanazotozwa kila mwezi wa mwezi Octoba mwaka huu.Katika kongamano na waandishi wa habari mjini Eldoret hii leo, kaimu katibu mkuu wa chama cha walimu nchini (KNUT) Lawrence Kahindi Majali alisema kuwa walimu wamesalia nyuma katika maendeleo kwa sababu ya [...]