Archive for the 'Fahamu Ya Fish' Category

Kibaki asema shuhuli ya kuundwa kwa katiba mpya mwananchi atashirikishwa kikamilifu

Tuesday, April 7th, 2009

Rais Mwai Kibaki amerejea nchini baada ya ziara rasmi ya siku tatu nchini Zambia.Rais Kibaki alilakiwa katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta na makamu wake Kalonzo Musyoka, naibu waziri mkuu Uhuru Kenyatta miongoni mwa viongozi wengine wa ngazi za juu serikalini.Akiwahutubia wakenya nchini Zambia, Rais Mwai Kibaki aliwahakikishia wakenya hao kuwa wananchi wote watashirikishwa [...]

Vijana wilayani Uasin Gishu wameombwa kulipa mkopo

Thursday, April 2nd, 2009

Vijana wilayani Uasin Gishu wameombwa kulipa mkopo ambao walipewa kutoka kwa hazina ya fedha ya maendeleo kwa vijana.Afisa anayesimamia maswala ya vijana katika wilaya ya Wareng David Mudhane amefichua kuwa ni kikundi kimoja tu cha vijana ndicho kimeanza kulipia mkopo kilichopokea mwaka jana.Mudhane alidokeza kuwa mkopo huo unapaswa kulipwa kwa muda Fulani huku vijana wengi [...]

Majaji wapya waapishwa

Thursday, April 2nd, 2009

Rais Mwai Kibaki amewasihi majaji wa korti ya kukata rufani na wale wa mahakama kuu kufuata sheria kikamilifu wanapotekeleza majukumu yao.
Akizungumza hii leo katika ikulu ya Nairobi katika hfla ya kuapishwa kwa majaji saba wapya, rais Kibaki alisema ana matumaini majaji hao watafuata sheria vilivyo na kuwahudumia wakenya bila uwoga, mapendeleo ama hila mbaya.Majaji hao [...]

Mutua ataka wakenya kuzingatia usafi ili kuzuia maradhi ya kipindupindu

Thursday, April 2nd, 2009

Msemaji wa serikali Dakta Alfred Mutua amewaomba wananchi kudumisha usafi wa hali ya juu ili kuzuia kusambaa kwa maradhi ya kipindupindu.Katika taarifa yake ya kila wiki kwa vyombo vya habari, Mutua alizitaka utawala za kimkoa kufunga vyumba vya kuuza vyakula ambavyo havizingatii hali ya usafi.Aidha amewataka wananchi kukumbatia mbinu za kujikinga ili kuepukana na maradhi [...]

Kamati simamzi ya serikali ya muungano kufanya mkutano wa faragha Tsavo wikendi

Thursday, April 2nd, 2009

Makamu wa rais Kalonz0 Musyoka amesema kuwa kamati maalum inayosimamia maswala ya serikali ya muungano itakuwa na mkutano wa faragha wa siku mbili Tsavo mwishoni mwa juma.Mkutano huo utakaofanyika hapo kesho na siku ya Jumamosi unalenga kuimarisha umoja katika serikali hiyo ya muungano ambao umekumbwa na hali ya kutoaminiana katika siku za hivi majuzi.Aidha mkutano [...]

Kanoute atia sahihi kandarasi mpya na klabu ya Sevilla

Thursday, April 2nd, 2009

Mshambulizi wa timu ya taifa ya Mali Frederic Kanoute amekubali kuongeza muda wa kandarasi yake na klabu anayechezea ya Uispania ya Sevilla.Hatua hiyo sasa itamweka kwenye klabu hiyo hadi mwaka wa 2012 kulingana na taarifa iliyochapishwa katika tovuti ya klabu ya Sevilla. Mshambulizi huyo matata atakuwa ameitimisha miaka thelathini na nne kandarasi hiyo itakapofikia kikomo [...]

Ahmed Hassan ateuliwa kuongoza tume huru ya uchaguzi nchini

Thursday, April 2nd, 2009

Ahmed Issak Hassan ameteuliwa kuchukua wadhifa wa uenyekiti wa tume huru ya mpito ya uchaguzi nchini-IICC.Hapo awali Hassan aliwahi kuhudumu kama mwanachama wa tume ya marekebisho ya katiba nchini.Akizungumza hii leo muda mfupi baada ya uteuzi huo kutangazwa na kamati teule ya bunge iliyotwika majukumu ya marekebisho ya katiba, Hassan alisema kuwa kamwe hatowaaibisha wakenya [...]

Fabregas akiri kufanya mazungumzo na aliyekuwa rais wa klabu ya madrid

Wednesday, April 1st, 2009

Nahodha wa klabu ya Arsenal Cesc Fabregas amekiri kufanya mazungumzo na aliyekuwa rais wa klabu ya Real madrid Ramon Calderon kwa simu.Calderon ambaye anapendezwa sana na kiwango cha usakataji soka wa Fabregas, kwa upande wake alisema alikuwa anamjulia hali mwanandinga huyo mzawa wa Uhispania jambo ambalo limewatia tumbo joto maafisa wakuu wa klabu hiyo.Fabregas mwenye [...]

orodha ya wanandinga wanaobugia donge nono duniani

Wednesday, April 1st, 2009

Jarida la France Football limetoa orotha ya wanandinga wanaobugia donge nono duniani huku kiungo wa kati wa Uingereza David Beckham ambae kwa sasa anasakata soka na klabu ya Milan kwa mkopo, akiongoza orodha hiyo.Nyota huyo wa uingereza anafuatiwa kwa ukaribu na wachezaji wenzake wa AC Milan Kaka na Ronaldinho.Moto wa kuotea mbali Chipukizi wa Argentina [...]

Malkia wa vituko Joyce Akinyi amegonga vichwa vya habari tena

Wednesday, April 1st, 2009

Malkia wa vituko Joyce Akinyi amegonga vichwa vya habari tena mara hii katika vuta nikuvute ya umiliki wa mkahawa wa deep west resort. Akinyi na aliyekuwa barafu yake wa moyo mzawa wa Naijeria Anthony Chinedu wanavutania mkahawa huo kila mmoja akidai kuwa mmiliki halisi.Sakata hiyo sasa imepanda daraja nyingine kwani sasa wanaoaminika kuwa familia ya [...]